click here

click here

Kichwa Bandia cha Trump chamtia matatani Mchekeshaji.

Kichwa Bandia cha Trump chamtia matatani Mchekeshaji Cathy Griffin.

Mwanamama Cathy Griffin ambaye ni msanii mchekeshaji raia wa Marekani alieonekana mubashara kupitia kipindi cha TV kinachorushwa na CNN akiwa ameshika kinyago kinachofanana kabisa na kichwa cha Rais Donald Trump, huenda akashtakiwa kutokana na kile kilichotajwa kama kuvuka mipaka ya Uhuru wa Habari.
Mwanamama huyo mwenye umri wa miaka 57 alionekana akiwa amebeba kinyago cha Rais Trump akiwa amekatwa kichwa, Jambo ambalo limezua hasira miongoni mwa raia wa Marekani pamoja na Rais Trump.
Msanii huyo alifukuzwa kazi  maramoja na  Kituo cha TV cha CNN ambacho  kilitangaza kufuta kipindi chake kuruka hewani.
Baadhi ya watu maarufu nchini Marekani akiwemo Rais Trump mwenyewe wamekilaani kitendo hicho na kusema ni dhihaka na udhalilishaji kwa familia za Wanajeshi na baadhi ya waandishi wa habari wa Marekani waliochinjwa na Kikundi cha kigaidi cha ISIS.
 
Kwa mujibu wa Idara ya Ulinzi wa Rais nchini Marekani (Secret Service) imesema kuwa uchunguzi umekamilika na wanajiandaa kumfikisha Mahakamani mchekeshaji huyo.

No comments

Powered by Blogger.