click here

click here

40 ya mtoto Jaden Yabum

40 mtoto wa Chuchu na Ray   Yabuma

Ni siku kadhaa sasa zimepita tokea siku ambayo wakali na mastaa wa filamu za Kibongo, Chuchu Hans na Vincent Kigosi ‘Ray’ kupanga kufanya shughuli ya kumtoa   Jaden  nje maarufu kama 40,kudaiwa kubuma, mwanamama huyo amefunguka kuwa licha ya kuchelewa bado ipo na inakuja ‘soon’. Chuchu aliongea hayo baada ya habari kuenea kuwa mastaa hao wameshindwa kumfanyia mtoto wao sherehe ya kumtoa nje ‘40’ kutokana na hali ya kifedha kuwa mbaya kwao.


“Ni kweli tumechelewa kumfanyia 40 mtoto wetu lakini ‘soon’ itafanyika tu na haya yote yanatokana na maamuzi ya baba yake ndiye aliyepanga hivyo siyo kukosa pesa kama wanavyodai, siku ya shughuli ikikaribia utasikia fununu tu,” alisema Chuchu.

No comments

Powered by Blogger.