click here

click here

Lissu afunguka kuhusu sakata la Mchanga wa Madini

Lissu afunguka kuhusu sakata la Mchanga wa Madini

  Tundu Lissu ambaye ni  Mbunge wa Singida Mashariki, kupitia tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),amesema kuwa msimamo wake wa kupinga kitendo cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli cha kuzuia mchanga wa dhahabu kusafirishwa nje uko pale pale.
Lissu amesema hayo alipokuwa  bungeni mjini Dodoma, aliongeza kwa kusema kwamba kuzuia mchanga huo wa dhahabu kusafirishwa kwenda nchi za nje kutaathiri uchumi kwani atakuwa ameenda kinyume na mikataba ya kimataifa.
“Rais Dkt. Magufuli amefanya kitendo ambacho ni kinyume na mikataba ya kimataifa, kwa hiyo hapa tutegemee hasara kubwa na kutengwa na jumuiya ya kimataifa,”amesema Lissu

No comments

Powered by Blogger.