click here

click here

TSJ Haikamatiki Kwa Wanahabari bora.

TSJ Haikamatiki Kwa Wanahabari bora.

     Na Nyamarasa Mgaya

   Bila shaka watu wengi wasomi na ambao hawajasoma wanaelewa kuwa Elimu ndiyo urithi pekee na bora kwa kila Mtu kuupata ili umsaidie katika maisha ya baadae.
   Elimu imezungumzwa na watu  tofauti katika jamii, wazazi, viongozi na hata vitabu vitakatifu kwa lengo la kuonesha umuhimu wake.
   Kumbe chanzo cha ufahamu wa mtu huanzia katika elimu na kuonekana katika jamii namna mtu huyo anavyofikiria na hata kimawazo na ushauri.
"Kila Mtu  anataka kufanikiwa lakini si kila Mtu yupo tayari kushika majukumu na wajibu wa kumpeleka kwenye mafanikio" alisema mwl Nyerere.

   Japo wengi huweka malengo ya kusoma sana na kupata elimu bora lakini hushindwa kutokana na kutokubali majukumu na wajibu wao.
   Mara nyingi kushindwa kutimiza malengo ya Mtu hutokana na kutofanya uchaguzi sahihi wa sehemu bora itakayosaidia kutimiza mafanikio yake.
   Uwepo wa Elimu bora Nchini ni matokeo chanya kwa Taifa kuwa na wasomi wenye fikra, mawazo, ujuzi na ushauri utakaowezesha  kusonga kwa maendeleo hapa nchini.
   Serikali yetu imekuwa ikilalamikia uwepo vyeti feki na watumishi hewa, kwa asilimia kubwa wengi wao walipata elimu isiyo bora na wengine kusoma katika sehemu ambazo hazina sifa.
   Suala hili linarudisha nyuma maendeleo ya Taifa na kwa Mtu binafsi, kuwa msomi bora kunaanza na sehemu utakapoita elimu hiyo.
   Kutokana na  harakati za kufanya uchaguzi wa sehemu bora itakayosaidia kutimiza lengo lako, tukabisha hodi katika chuo cha uandishi wa habari cha Tsj.
   Chuo hiki ni moja kati ya vyuo vikongwe katika ufundishaji wa taaluma ya uandishi wa habari na utangazaji hapa nchini.
   Time school of journalism (TSJ) kilianzishwa rasmi mei 15 mwaka 2000 katika eneo la msimbazi center kikisimamiwa na watu binafsi walioungana na kuanzisha kama taasis iliyoitwa  "time" (Tanzania institute of media education).
   Tangu kuanzishwa kwake kimekuwa kikikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo za kifedha na majengo lakini bado kimeendelea kudumu na kuwa moja  kati chuo chenye sifa kubwa.
   Taarifa zilizotolewa na mkuu wa Chuo Bi Suzana Lucas zinaeleza kuwa katika vituo vingi vya Habari hapa nchini vina wafanyakazi waliosoma Tsj.
   Bi Suzana aliongeza kuwa chuo hicho kimeweza kutoa waandishi wengi wa habari hapa nchini na kimataifa, Salim kikeke mtangazaji wa BBC akiwa ni mmoja wa wanafunzi wa Tsj.
   Kufanikiwa kwa mtu ama taasis hukamilika pale anapojiwekea malengo na kuyasimamia ipasavyo ili yatimize  mafanikio aliyokua akiwaza namna ya kuyatimiza.
   Pia Tsj ilipoanza ilikuwa na malengo mazuri ambayo yamefanya kudumu katika ushindani wa vyuo vingi vya Habari nchini.
   Mkuu wa Chuo cha Tsj Bi Suzana Lucas alieleza kuwa shauku yao ni kutoa wanahabari bora watakaoweza kufanya kazi zao kwa kujiamini kwa kufuata taaluma walioipata.
   Chuo hiki kipo cha ya wakurugenzi ambao majini yao tumeyahifadhi na wanasimamia na kuhakikisha shughuli za ufundishaji na mambo mengine yanaendelea kama kawaida.
Tsj ni moja kati ya vyuo vya Habari vinavyoamiwa hapa nchini katika kutoa mafunzo ya uandishi bora wa habari na utangazaji kitaifa na kimataifa.
   Huenda msomaji unaesoma makala hii ulikuwa ukiwaza ni chuo gani unaweza ukasomea ama akamuelekeza ndugu yako na hata rafiki yako ili akasomee taaluma ya habari bila shaka umepata jibu sahihi
   Ili Taifa lisonge mbele kimaendeleo lazima lipate waandishi bora wa habari watakaoweza kuibua mambo yaliyojificha katika jamii na taasis mbalimbali za umma.
   Kutokana na tamko la serikali kupitia waziri wa Habari, utamaduni, sanaa na michezo mh Harrison mwakyembe kuomba wanahabari kusoma na kuhakikisha japo mwandishi wa habari kuwa na Elimu ya stahada, Tsj inawakaribisha  wanahabari kujiunga na chuo hicho.
   Chuo cha Tsj kwa sasa kinasajili wanafunzi mia 3 kila mwaka ikiwa ni ongezeko kubwa ikilinganishwa na wanafunzi 6 kilichoanza nao mwaka 2000.
   Pia kina mpango wa kujenga majengo yake binafsi katika eneo la Bunju jijini Dar es salaam na kuachana na upangaji katika majengo ya watu binafsi.
   Chuo cha Tsj kinapatika katika eneo la Ilala bungoni jijini Dar es salaam na kinatoa taaluma ya uandishi wa habari kwa ngazi ya astahada na stahada pekee.
   Ili uwe na Elimu bora itakayosaidia kutimiza malengo yako lazima utafute chuo bora kitakachosaidia kumiza ndoto yako, maamuzi yako ya Leo ndiyo mafanikio yako ya kesho.

No comments

Powered by Blogger.