Shamsa Ford Amuoneaa Wivu Odama
Shamsa Ford Amuoneaa Wivu Odama
Mwanadada anayefanya vizuri kwenye tasnia ya filamu Nchini, Shamsa Ford amefunguka juu ya kuonea wivu mahusiano
ya muigizaji mwenzake, Jenipher Kyaka 'Odama' kwa kuyafanya kuwa na
usiri mkubwa huku akipongeza na kusema ndivyo inavyopaswa mtoto wa kike
kufanya kwenye mapenzi.
Shamsa amesema hayo alipotoa maoni yake katika ukurasa wa instagram wa Odama na kufunguka kuwa anapenda jinsi muigizaji huyo
anavyoweza kuweka mahusiano yake ya mapenzi kuwa faragha yake peke yake
na kuongeza kuwa anatamani kama siku zingerudi nyuma asingethubutu
kumuonyesha mpenzi wake hadharani bali mume wake wa ndoa.
Shamsa amesema hayo alipotoa maoni yake katika ukurasa wa instagram wa Odama na kufunguka kuwa anapenda jinsi muigizaji huyo
anavyoweza kuweka mahusiano yake ya mapenzi kuwa faragha yake peke yake
na kuongeza kuwa anatamani kama siku zingerudi nyuma asingethubutu
kumuonyesha mpenzi wake hadharani bali mume wake wa ndoa."Napenda unavyoweka mahusiano yako ya mapenzi 'private'. Sijawahi ona hata siku moja umempost sijui boyfriend na hicho ndo kitu kizuri kwa mtoto wa kike. Mimi kwa upande wangu ningerudisha siku nyuma kipindi kile nipo single nisingempost au kumuweka wazi mwanaume yoyote niliyekuwa naye kipindi kile kwenye mahusiano. Natamani mume wangu ndio angekuwa mwanaume wa kwanza kwa watanzania kumjua" - Shamsa Ford alifunguka.

Post a Comment