click here

click here

MOON JAE IN, RAIS MPYA WA KOREA KUSINI, MWENYE MALENGO MAZURI NA KIM JONG UN



MOON JAE IN, RAIS MPYA WA KOREA KUSINI, MWENYE MALENGO MAZURI NA
 KIM JONG UN
Na Erick Paschal,TSJ
erickpaschalkavishe@gmail.com
    Ni wiki kadhaa zimepita tangu Moon Jae in achaguliwe kuwa Rais mpya wa Taifa la Korea Kusini, ameshinda kwa kishindo na kuwa Rais wa 12 wa Taifa hilo na kuziba pengo la aliyekuwa Rais wa taifa hilo Bibi Park Geun hye, aliyejiuzulu kwa kushinikizwa na wananchi wa Korea kwa tuhuma za ufisadi toka mwishoni mwa Januari,2017.
                           


Rais wa Korea Kusini Bwana Moon Jae In. (Picha kwa msaada wa mtandao wa Wikipedia)
    Bwana Moon ameonekana kuwa na mtazamo tofauti kuliko inavyotegemewa na raia wengi wa Taifa hilo lililopo Barani Asia. Kubwa alilolinadi Rais huyu mpya, ni kuimarisha kwa mara nyingine uhusiano wake na Korea Kaskazini, Taifa ambalo limekuwa na mgogoro wa muda mrefu na Taifa hilo. Kitu kilicho kinyume na sera za taifa hilo kwa muda mrefu. Bwana Moon anataka kupunguza na ikiwezekana kuondoa kabisa uhasama uliopo kati ya Korea kusini na Korea Kaskazini.
   Lakini si jambo hilo tu linaloishtua Dunia kwa sasa, kwani mara baada ya kuapishwa Bwana Moon, amehoji mfumo wa ulinzi wa Marekani na kuhoji ni kwanini Marekani iliweka makombora ya Ulinzi katika ardhi ya nchi yake. Kitu ambacho wengi wao hawakukitegemea kwani Marekani na Korea Kusini wamekuwa washirika wakubwa tena wakiwa bega kwa bega kupingana na Korea Kaskazini. Ambayo imekuwa ikirusha makombora ovyo kwa nchi jirani kama vile Japan pamoja na Korea kusini. Rais Moon Amekaririwa na Vyombo vya Habari mbalimbali akisema atapenda kuitembelea Pyongyang katika hali nzuri.
    Hatahivyo Rais Moon amesema atashughulika sana kuliunganisha Taifa hilo linalokabiliwa na ufisadi ambao ulisababisha mtangulizi wake kushitakiwa, mbali na kulipa kipaumbele swala la kuimarisha Uchumi wa Taifa hilo.
Pia Bwana Moon ana mpango wa kutenga zaidi ya dola billion 8.9 kuinua ajira katika taifa hilo, malengo yake ni kuanzisha ajira zaidi ya laki nane na kumi kwa vijana wa Korea kusini.
   Lakini raia wengi wa nchi hiyo wameonekana kuwa na wasiwasi na Kiongozi huyu mpya, juu ya kuungana na Korea Kaskazini kwani wananchi wa Korea Kusini wanahisi kuna uwezekano wa vita kujirudia tena katika harakati za kuungana. Kwa upande wa vijana ambao wengi wao ni wasomi wa elimu ya juu, wanaona suala hili linaweza kuliingiza rasmi vitani nchi hiyo na jirani yake Korea Kaskazini.
TUTAZAME MAISHA YAKE BINAFSI
      Ana umri wa miaka 64, amezaliwa Januari 24 mwaka 1953 katika eneo la Geoje, ni mtoto wa kwanza kwenye uzao wa baba yake ajulikanaye kwa jina la Moon Yong-hyung na mama yake Kang Han-ok. Baba yake alikuwa ni mkimbizi kutoka Kusini mwa Hamgyeong province ambalo kwa sasa ni eneo la Korea ya Kaskazini, ana mke mmoja afahamikaye kwa jina la Kim Jung-sook, na ni baba wa watoto wawili.
    Kitaaluma ni Mwanasheria, pia ni mwanaharakati wa haki za binadamu. Amewahi kufaulu elimu ya juu zaidi kuhusiana na masuala ya sharia, lakini hakuweza kupandishwa cheo na kuwa jaji wa mahakama au Mwendesha mashitka wa Serikali kutokana na harakati zake za haki za kibinadamu  alizozifanya, ili kupingana na udikteta wakati akiwa ni mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Kyung Hee. Ndipo akaamua kubaki kama wakili au mwanasheria, pia amehudumu kwa nafasi mbalimbali katika taifa hilo. Amewahi kuwa Katibu Mkuu wa Ikulu kipindi cha Raisi Roh Moo-hyun machi 2007 mpaka Februari 2008, Rais Moon pamoja na Rais Roh, kimahusiano walikuwa ni marafiki. Bw. Moon alikuwa mtu wa karibu na Rais huyo kabla ya Rais huyo wa zamani wa Korea Kusini kujiua mwenyewe Mei 23 mwaka 2009 akiwa na umri wa miaka 62.
  Rais Moon Jae-in ni muumini mzuri wa dhehebu la kikatoliki na kiongozi wa pili kutoka katika Dini ya kikristo ukiachana na Rais mstaafu Kim Dae-jung.

No comments

Powered by Blogger.